Fadhila za kueneza na kudhihirisha maamkizi ya kiislamu

Amesema Mtume (s.a.w): ''Hamtaingia peponi mpaka muamini, na hamtakuwa waumini wa kweli mpaka mpendane. Hivi niwafahamishe kitu mkikifanya mtapendana? Salimianeni baina yenu.''

Amesema Ammar bin Yaasir (r.a): 'Mambo matatu anaeyakusanya basi amekusanya Imani, uadilifu wa nafsi yako, na kutoa salamu kwa watu wote, na kutoa (sadaka) hali ya kuwa ni mchache wa mali.'

Imepokewa kutoka kwa Abdallah bin Omar (r.a) kwamba mtu mmoja alimuuliza Mtume (s.a.w): 'Ni uislamu gani bora? Mtume (s.a.w) akamjibu: Kulisha chakula (masikini) na kumsalimia unaemjua na usiemjua.''

API